Sayari Saba - Massimo Longo E Maria Grazia Gullo 2 стр.


"Tuacheni." akamrishwa Ruegra.

Alisalia pekee akiwa na adui mwenye akili kali. Alikumbuka kuwa wakati wa vita alikuwa ameweza kubadilisha hali mbaya ambayo ilikuwa imetabiri kifo chake, shukran kwa kufikiria kimkakati na licha ya kuwa na watu wachache kutoka Sayari ya sita chini ya utawala wake.

Alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kuzungumza. Alikuwa tayari amewaza kuhusu mikakati kadhaa wakati wa safari yake. Alijua kwamba haingewezekana kumshika adui yake bila kufahamu. Ilikuwa wakati wa kuchukua mmoja na kuanza makabiliano.

Aliamua kuendelea na ibada hiyo ya kumsifu akitarajia kwamba uzee wake na uchovu wake umemfanya kudhoofika zaidi.

"Nakusalimu, Wof. Ninaweza kusema kwamba hauonekani vibaya licha ya kutopewa matibabu bora. Hata hivyo nimeamrisha upatiwe vitabu na elimu. " "

"Muda mrefu sijakuona." alisema Wof, akimtazama jenarali huyo na macho yake ya kina na meusi. "Ni nini kilikuleta mahali hapa ambako imesahaulika na mwangaza, ambako giza inatawala?"

"Nilikuja hapa kuongea nawe kuhusu baba yangu. Nakumbuka kuwa nikiwa mtoto angefikria kuhusu Ngozi ambayo ulijua siri zote kuihusu. Sasa kwa kuwa ninazeeka, wakati mwingine ninafikiria kumhusu na kushangaa iwapo kuna ukweli kuhusu hadithi hiyo."

Wof alijaribu kuficha ushangao wake kwa kupapasa nywele zake hizo ambazo zilikuwa zinampa sura uso wake nyeusi.

"Baba yako alikuwa akisema ukweli, lakini inavyoonekana, hakufikiria kwamba ulikuwa mwaminifu wa kutosha kujua maelezo yote.

Pia alijua siri zote ambazo hazijazungumziwa. Ruegra alishangaa. Baba yake alikuwa ametaja siri hiyo mara nyingi, lakini hakuwahi kuwa na hamu ya kufichua.

"Nini mbaya, Jenerali? Unashangaa kwanini hakukuambia zaidi kuihusu?"

"Labda umri wangu mdogo na msukumo wangu ulinifanya msikilizaji mbaya."

"Afadhali niseme kwamba tabia yako ni hamu ya kuwa na mamlaka na utawala wa kijeshi."

"Mamlaka ni muhimu kudumisha utulivu na uimara." Akasisitiza Jenarali huyo, baada ya kusimama akiwa amekasirika.

"Una imani na utaratibu, ukiwa umeajiriwa kuhudumia mtu mmoja na kwa utulivu wa kabila moja." akajibu Wof.

Ruegra alianza kutembea kwa uwoga. Alikuwa tayari amepoteza uvumilivu wake, lakini alijua vizuri kuwa hakuna mateso au ulafi ambao ungefanya kazi kwa mtu ambaye alikuwa ameketi mbele yake. Tumaini lake la pekee lilikuwa kupata uaminifu wa mtu huyo.

Alianza kuwa mjanja na kudanganya:

"Unajua, kwa kweli ninamheshimu baba yangu. Wakati nilipokuwa mdogo ulikuwa ukisema kwamba ninafanana naye... Wakati huo, nilikuona kama bwana...."

"Nini inakufanya kufikiria kwamba nitafichua jinsi ya kupata ngozi hiyo? Usafi huo uliokuwa nao utotoni ulipotea haraka, Ruegra, na nia ya kujithibitisha ilichukuliwa na kiu ya mamlaka."

"Mimi si Aniki ambaye unamkumbuka wakati wa vita. Nitajua kuthibiti mamlaka kwa usawa. Baba yangu alifanya makosa kwa kukosa kuniambia kila kitu." "Jenerali alisema kwa hasira nyingi.

"Ikiwa ilibidi uje kwangu, inamaanisha kuwa haukustahili kuaminiwa na baba yako. Ni baba wa aina gani anayeficha maarifa kutoka kwa mwanawe? Kuna taabu katika ishara zake. Nani aliyebora kuliko yeye alikujua na mimi ni nani kufichua kila kitu kwako na kupuuza kabisa tathmini yake? Kama unavyoona siwezi fanya chochote lakini kuheshimu nia yake na kuheshimu kumbukumbu yake." Alisema Wof. Kisha alisimama na kusema kwaheri kwa mnyongaji wake.

Tukio hilo halingeondoka katika akili ya Jenarali, ambaye aliendelea kutazama angani akiwa na glasi mkononi kwenye usiku huo wa Bonobo uliokuwa joto.

Asubuhi iliyofuata, Ruegra alichunguza binafsi kazi ambayo ilikuwa imekamilishwa kubadilisha sehemu iliyoharibika ya chombo cha angani.

Mastigo alikuwa amefuatilia vizuri na mafundi wake walikuwa wamefanya kazi nzuri kama kawaida. Wakaondoka kwa wakati uliowekwa na kurejea nyumbani.

Siku zilikuwa zikipita na Ruegra alikuwa na haraka ya kurudi nyumbani. Aliogopa njama, ingawa kakaye, ambaye alikuwa akiongoza wakati hakuwepo, atampa Jenarali ripoti za kila mara kuhusu hali hiyo. Hapakuwa na kitu cha kuwa na wasi wasi nacho. Carimea ilikuwa mchanganyiko wa jamii. Makabila tofauti walikuwa wakipigania utawala dhidi ya Wa-aniki, lakini Wa-aniki walikuwa wamewaondoa idadi inayodhihirika ya wapinzani wakati wa utawala wao. Ilikuwa imeanzishwa na vikundi kadhaa vya mfumo tofauti wa jua, wengi wao walikuwa watalii, watafutaji wa bahati au wafungwa wa awali ambao walikuwa wakitafuta ardhi kuanzisha maisha yao upya. Sehemu ndogo tu kati yao walitoka kwenye sayari hiyo. Kwa kweli, watu wa sehemu hiyo walikuwa wametawaliwa kishenzi na kutengwa.

Njiani wakirudi, huku akiwa ameketi katika kiti cha kuthibiti chombo kwenye dashibodi, Ruegra alikuwa akifikiria kuhusu maneno ya Wof. Kwamba "Baba yangu alijua" iliendelea kusikika akilini mwake.

Kisha kwa ghafula, akafikiria nyakati zote baba yake angeondoka wakati wa msimu wa uwindaji na kabla ya vita vyote. Mahali alipenda kwenda ilikuwa kwa kweli ardhi ya Bonobo, haswa kwa Bahari ya Unyamavu.

Wakati fikra hizo zilikuwa zikitembea kwenye akili yake, alipata utambuzi wa kuangaza na kufikira:" Mbona sijafikiria kuhusu haya awali?" Kitu au mtu huku huenda alimpa taarifa zaidi kuhusu ngozi hiyo iliyo na siri.

Alihusisha uhisi wake na ripoti ya Mastigo kuhusu chombo cha angani cha kibiashara. Labda mtu alikuwa mbele yake.

Aliamuru kubadilisha njia mara moja. Walikuwa wanarejea huko Bonobo.

Mastigo, aliyekuwa ameshangaa baada ya kuwaona wakirudi, alikimbia kuelekea chombo hicho cha angani.

"Ninasalimu mtu ambaye hawezi kushindwa miongoni mwa watu wa Carimea. Jenerali, mbona umerudi?"

"Nimetafakari kuhusu kutua kwa chombo hicho cha angani, na imenishawishi kurudi na kushughulikia binafsi hali hiyo."

"Kwa mara nyingine, umefanya jambo la busara. Wataarifu wangu hawakurejea Bonobo. Kwa hivyo, niliamua kuzuru eneo hili mimi binafsi. Niligundua kuwa walikuwa wameondolewa na watu wasiojulikana."

Ruegra alikuwa akitumaini kuwa Gavana wake hajaharibu uwezekano wote wa kupata taarifa kwa kuwa alijua njia zake.

"Hakuna kilichoachwa huko." akaripoti Mastigo mara moja, ambaye alikuwa akionekana kuridhika kama mtoto ambaye alitesa mawindo yake madogo.

Ruegra alijizuia kumshambulia msemaji wake na kumwuliza mahali wafanyakazi wake walikuwa wameenda.

Mastigo alichukua pumzi mzito, akifahamu kuwa haitakuwa Habari njema.

"Hatukuweza kuipata. Lazima wamekimbia."

"Sio tu uliharibu ushahidi wote, lakini pia uliwaacha wafanyakazi kutoroka! Ulikuwa huna ujuzi wewe! Nipeleke huko!"

Kisha, baada ya kufikiria tena alitambua kuwa haitakuwa wazo nzuri kumruhusu Mastigo kufahamu kuhusu mipango yake.

"Niandalie wafanyakazi. Nitaondoka kesho bila wewe."

Sura ya Pili

Upanga wa jiwe ulikuwa ukining'inia juu ya vichwa vyao.

"Tujiandae? Huenda tusikaribishwe tukapowasili! "alishangaa Oalif, ambaye ni mwerevu zaidi kwenye kundi hilo.

Wafanyikazi walijumuisha wanachama wanne kutoka sayari ambazo zilikuwa zikipambana dhidi ya utawala wa Carimea. Walichaguliwa kwa sababu ya historia yao ya matumizi na pia uwezo wao wa mwili na akili. Kwa pamoja wangeunda timu ambayo ingeweza kufanya kazi yoyote, nyingi na kimkakati. Wajibu wao ulikuwa kuhakikisha amani na sio tu hatua za kijeshi, lakini pia shughuli zinazohusiana na ujasusi na uratibu kati ya watu tofauti.

Baraza la Muungano wa Sayari Nne lilikuwa limewateua kuwa "Tetramiri", ambayo ilimaanisha kwamba wanaweza kufaidika na Serikali kutoka kwa mamlaka maalum na kazi hadi kukamilika kwa utume wao.

Meli ndogo cha angani cha kibiashara kilikuwa kikivuka miviringo mikubwa za kijivu za Bonobo na kilikuwa kikiendelea kuelekea Bahari ya Ukimya.

Meli ndogo cha angani cha kibiashara kilikuwa kikivuka miviringo mikubwa za kijivu za Bonobo na kilikuwa kikiendelea kuelekea Bahari ya Ukimya.

Aina hiyo ya chombo cha angani ilitengenezwa kwa minajili ya usafirishaji wa bidhaa. Iliumbwa kama mabomba sambamba yaliyo na kingo zilizobutu mbele ili kutoa mwendo mzuri angani. Juu ya hayo, ilikuwa wameweka mabawa madogo, yanayoweza kutolewa ambayo yalitumika wakati wa kuvuka anga. Nyuma, kulikuwa na mlango mkubwa wa kushikilia ambao ungefunguliwa katika sehemu tatu kama taji ya maua na ilitumika wakati wa kupakia na kupakua. Vyombo hivyo vya angani vilikuwa kubwa na mwendo wa polepole. Vingeondoka na kutua sambamba na ardhi bila hata kuacha nafasi yoyote ya badiliko la mwelekeo wa mapigo, kama vyombo vingine vile vya angani.

"Jitangaze." sauti ya metali ilitoka redioni.

"Sisi ni wafanyabiashara, bwana." alijibu Oalif.

"Tunaweza kuona. Lakini ni nani na ni nini mmebeba? Una leseni? "

"Settimo kutoka Oria, bwana."

"Nambari ya leseni, sasa!" alisisitiza mlinzi.

"34876."

"Wewe haumo katika orodha yetu. Badilisha njia mara moja. Huna ruhusa yoyote ya kutua katika eneo hili. "

"Mawimbi ni dhaifu, bwana. Sikusikii. Leseni namba 34876. "alisema Oalif kwa mara ya pili, akijifanya hasikii kile mlinzi alikuwa anasema.

"Ruhusa ya kutua imekataliwa!"

"Hatuwezi kunakili wewe, bwana." alisisitiza mtu huyo wa Bonobo kisha akawaambia wafanyakazi wake akisema: "Tuko ndani, jamani! Tunavuka ukungu katika Bahari ya Ukimya! "

Oalif alikuwa rubani mzoefu, na akiwa Bonobo, alikuwa mjuzi wa kiwango cha juu wa sayari yake ya asili. Walakini, hakuendana na tabia rahisi na nyepesi ambazo kawaida zilipewa kabila hilo. Kabila lake lilikuwa halijawahi kutolewa kwa Waaniki, na kwa sababu hiyo lilikuwa limelipa bei kubwa. Wakati wa vita vya mwisho, baada ya kupoteza udhibiti wa sayari yao wenyewe, walikuwa wamehamishwa na kushikiliwa na Muungano wa sayari, ambao walikuwa wakipanga maandamano ya ndani. Lengo lao lilikuwa kupata tena udhibiti wa sayari.

Mwili wa Oalif ulikuwa na nywele nyeusi za mwili ambazo hazingeonyesha ngozi yake nzuri. Eneo tu linalozunguka macho yake ya kijani na mashavu yake hayakuwa na nywele. Alikuwa na ndevu nene, zilizochongoka, ndefu hadi kifuani, na angeweka nywele zake ndefu kama mkia wa farasi nyuma ya shingo lake.

Oalif alikuwa mtu anayefaa kwa utume huo, lakini kwa bahati mbaya, angelazimika kukaa ndani ili asije akaonekana. Kwa kweli, alikuwa akitafutwa: uso wake ulijulikana sana, na hawakujua watakutana na nani au nini.

Meli ya angani ilitua katika eneo la kijani kibichi, lenye jua lililovukwa na mto mpana na maji ya kina kirefu na safi ambayo yangeonyesha sakafu ya mto. Mwisho huo ulifunikwa na aina mbali mbali ya mawe, kama vile kwenye picha ya mtaalam wa maoni.

"Njia bora ya kuficha kitu, ni kufanya hivyo hadharani. Oalif, washa mtambo wa kuficha mara tu tunaposhuka. Asante, umekuwa mzuri. "Alimpongeza Ulica, wa Eumenide.

"Mahali hapa ni pa ajabu. Mara tu unapoingia ndani, ukungu unaozunguka hupotea na miale ya KIC 8462852 huanza kutia joto angani kana kwamba ilikuwa majira ya joto. "Aligundua Zàira kutoka Oria mara tu alipotua.

"Harakisha. Tuna muda mdogo wa kupata makao kabla ya jioni. Mastigo hatatuachia wakati mwingi wa kutafuta nyumba ya monasteri "aliamuru Xam kutoka Sayari ya Sita, ambaye alikuwa mshiriki wa nne wa kikundi hicho.

"Wacha tufuate mkondo wa mto." alipendekeza Zàira. " Msitu unaouzunguka utatufunika wakati tunachagua njia inayofaa zaidi. "

Walijitosa msituni. Xam na Zàira walikuwa wakiongoza njia wakati Ulica alikuwa akitafuta njia sahihi ili kufikia kijiji cha Bonobo. Huko walikuwa wanapanga kupumzika na kupata habari zaidi kuhusu monasteri ya Nativ, lengo lao kuu.

Xam, shujaa kutoka Sayari ya Sita, alikuwa mwanadamu ambaye alikuwa amesimama wakati wa vita kwa ujasiri wake na ubinadamu.

Alikuwa kijana mrefu, mwenye misuli. Alikuwa na ngozi nzuri na nywele fupi nyeusi, zilizokunjika. Midomo yake kamili ilikuwa imefichwa na ndevu nene zilizonyooka. Juu ya suruali yake nyembamba, alikuwa amevaa mkanda wa teknolojia wa kazi nyingi ambao ulibuniwa na watu wake ili kupata hali bora maishani au kifo. Pande nyingine ya mwili wake ilifunikwa na jeli iliyotumiwa na watu wa Sayari ya sita kudumisha hali ya joto ya mwili katika hali yoyote ya hali ya hewa.

Zàira, ambaye alikuwa rika lake, alitoka Oria, sayari yenye anga finyu. Silaha nyeusi, ya asili ilifunikwa mwili wake, kuanzia juu ya paji la uso wake na kunyooka nyuma hadi mkia wake: ilikuwa tabia ya kabila hilo. Sufi fupi na nene ilifunikwa mwili wake wote, isipokuwa uso wake kama wa kibinadamu ambao macho mawili ya kijani kibichi yenye kupendeza yalisimama. Kwenye paji la uso wake, kwa pande za silaha alikuwa na vifungu viwili ndefu vya nywele nyeupe ambazo kwa kawaida angefunga kwa kusuka hadi mabegani.

Ulica, mdogo kati ya hao wanne, alikuwa mwanasayansi ya kiwango cha juu na mtaalam wa hesabu kutoka Eumenide. Alikuwa wa tabaka wa juu na wa kifahari kama kipepeo. Mwili wake ulikuwa umefunikwa kwa johari ya uwazi pazia la asili ambayo ilionekana kama mabawa ya kipepeo.

Kwa kufungua mikono yake, mabawa yake yangeenea wazi na kumruhusu aruke. Yalikuwa yamekunjwa na kushushwa chini nyuma ya mikono yake. Yalionekana kama tatoo ya henna: vipande nyembamba, vya hariri ambavyo vingeweza kunyoosha na kutumiwa kama lasso au mjeledi.

Jaribio hilo lilidumu kwa muda mrefu kuliko kawaida kwa sababu ya hitilafu kwenye kifaa cha ufuatiliaji iliyosababishwa na athari nyingine ambazo zilikuwa zikitokea katika vifaa kwenye Bahari ya Ukimya. Tukio hilo lisilotarajiwa liliwafanya waachane na njia sahihi kando ya ziwa na kusababisha ucheleweshaji wa siku chache katika mpango wao.

Baada ya kugundua shida, walijikuta wakirudisha hatua zao na wakakimbia kando ya kijito hadi walipoona ukanda. Macho yao yaligundua safu ya vibanda vidogo vilivyopangwa kwa duara. Katikati kulikuwa na sangara inayotumika kupika wanyama wa porini. Kuta hizo zilijengwa kwa shina kubwa, la mianzi ambalo lilikuwa limefungwa pamoja na kufungwa na tope na nyasi zilizopasuliwa. Paa hizo zilitengenezwa kwa majani ya mitende yaliyofumwa pamoja. Kwenye ncha kulikuwa na shimo ambalo lilitumika kama mahali pa moto, ambalo lilifunikwa na muundo zaidi wa umbo la koni.

Kwa mshangao wao mkubwa waligundua kuwa kijiji kilikuwa karibu na eneo la kutua kuliko ilivyotarajiwa.

Baada ya kuona wageni, wakaazi wote walitoroka, wakijificha katika vibanda vyao. Walionekana karibu kama mipira ya mchezo wa pool inayopigwa na mpira wa kuanza mchezo.

Walijikuta mbele ya kabila moja la mwisho la Bonobo ambalo lilikuwa halijatawaliwa na Waaniki kwa kupata makazi katika eneo kama hilo lenye uhasama.

Wanne hao hawakufanikiwa, hata hivyo, kwenda bila kuonekana. Baada ya sekunde chache wapiganaji wenye silaha na mikuki walijitokeza mbele yao.

"Tunakuja kwa amani." akasema Xam kwa haraka.

"Tunataka pia amani." alisema mpiganaji aliyekuwa na kitambi kubwa, ambaye alionekana kama bosi.

"Kwa sababu hii, tunataka uondoke!"

"Hatutafuti shida. Lakini tunahitaji msaada wako. Oalif alizungumzia ujasiri wako. "

"Oalif alituacha miaka mingi iliyopita. Kwa nini umekuja hapa? "

"Tunatafuta nyumba ya watawa ya Nativ."

"Kwa nini?"

"Tuko kwenye ujumbe wa amani ambao unahusisha watu wote."

"Wengi wamekuja hapa kwa kisingizio cha amani, lakini basi waliishia kusababisha vita tu."

"Lakini kama unavyoona, sisi sio Waaniki. Mimi ni Xam wa Tetramir. Lazima umesikia kutuhusu...

"Xam kutoka Sayari ya Sita?"

Xam aliguna.

"Nenda ukamwite yule mwenye busara." aliamuru mpiganaji huyo mwenye kitambi.

Назад Дальше